Rais mteule nchini Marekani Donald Trump amethibitisha kuwa mkuu wa kampuni ya Exxon Mobil, Rex Tillerson ndiye waziri wa mambo ya nje nchini Marekani.
Bwana Trump alimsifu Tillerson mwenye umri wa miaka 64 kama mmoja wa viongozi wa biashara wenye tajriba kubwa zaidi duniani.
Bwana Tillerson anatajwa kuwa na uhusiano mwema na rais wa Urusi Vladimir Putin jambo ambalo limewatia wasiwasi wa wanachama wa Democratic na baadhi ya wale wa Republican ambapo uteuzi huo unahitaji kuthibitishwa na bunge la Senate.
Siku chache zilizopita ilibainika kuwa majasusi nchini Marekani wanaamini kuwa Urusi ilihusika na kushawishi ushindi wa Trump.
Waziri wa mambo ya nje wa nchini Marekani ndiye mwanadiplomasia wa cheo cha juu zaidi ambaye uhusika na sera za kigeni za nchi.
Warning: file_get_contents(http://graph.facebook.com/?ids=http://habarika.com/trump-amteua-mfanyabiashara-mwenzake-kuwa-waziri-wa-mambo-ya-nje-ya-marekani/): failed to open stream: HTTP request failed! HTTP/1.1 403 Forbidden in /home/habarika/public_html/wp-content/themes/habarika/elements/element.php on line 80
0 comments